Jumatano, 24 Oktoba 2018

MALKIA WA USHUHUDA DR TUMAIN MSOWOYA AWAGUSA WENGI

MALKIA WA USHUHUDA DR TUMAIN MSOWOYA AWAGUSA WENGI
Mariam kilyenyi amtaja Dr Tumaini msowoya kama Malkia wa ushuhuda Tanzania asema nyimbo zake na harakati zake Dr Tumaini zimejaaa ushuhuda mwingi ambao umegusa watanzania wengi
Pichani akionekana MWIMBAJI MARIAM KILYENYI akiwa na DR TUMAIN MSOWOYA katika hafla fupi ya kuwania tuzo.
Kwa ufupi: MWIMBAJI MARIAM KILYINYI ni MWIMBAJI anaye sifika kwa. Jina la MAMA WA UPENDO
Kutokana na kawaidayake ya kuwapenda na kuwapa ushilikiano Mkubwa waimbaji wenzake na sasa MWIMBAJI huyu anakaribia kuzindua album yake Mpya tarehe 02/mwezi 12 /mwahahuu 2018 dani ya kanisa la KKKT SINZA jiji la dar es salama na inataraji kuwa siku kubwa na ya kipekee kutokana na upendo wake kwa waimbaji wenzake
watu mashuhuri kutoka nje na ndani ya nchi wameendelee kudhibitisha kuwepo sikuhiyo ikiwemo UTUKUFU LABEL kutoka nchini ZAMBIA ambapo ndani yake kuna waimbaji kutoka KENYA, NIGERIA, na AFRICA YA KUSINI

FAIDA KUMI NA MBILI ZA MAOMBI

MOJA: Maombi yanaimarisha uhusiano wa mtu na Mungu; Maombi ni mawasiliano baina ya mwanadamu na Mungu au ni njia ambayo tunaweza kuwasiliana na Mungu. Naamini unafahamu kuwa mawasiliano yanaongeza uhusiano wa mtu na mtu, hata wewe ni shahidi katika hili unaweza ukawa na ndugu wengi sana au marafiki wengi sana lakini yule ambaye anawasiliana na wewe mara kwa mara huyo ndiye anayeukuza ukaribu baina yenu kuliko wengine.
Ukweli wa mambo ni kwamba uhusiano wa mtu na mtu unaanzishwa kwa mawasiliano na vile vile unaweza ukapungua au hata ukafa kabisa kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara. Mawasiliano ndio yanayofanya mahusiano yawe hai na yenye afya na ndio yanayowafanya watu wengi kuwa karibu. Tunapokuwa tunaomba mara kwa mara uhusiano wetu na Mungu unakuwa kwa kasi sana kuzidi yule asiyeomba, au yule anayeomba mara moja moja au yule anayeomba kwa viwango vya juu zaidi. Na kama tujuavyo, kadiri uhusiano wa mtu na mtu unavyokuwa na kuongekezeka ndivyo wanavyoweza kushirikishana mambo mengi zaidi.

MBILI; Maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu aliyoyapanga kwa taifa au kwa mtu ili afanye sawa sawa na vile wewe unataka lakini sawa sawa na kusudi lake; “Siku hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona. Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana akasema, Nakusihi, Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana. Ikawa, kabla Isaya hajatoka katika mji wa kati, neno la Bwana likamjia, kusema, Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana.” (2 FAL. 20:1-5). Hezekia alijua aljua na aliamini kuwa maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu la sivyo asingeomba. Soma pia Yona 3:1-10.
Kama maombi yanaweza kumshawishi Mungu kubadilisha maamuzi basi maombi yanaweza kutumika kubadilisha maamuzi ya mtu, ipo mifano mingi ya kibiblia inayoelezea juu ya maamuzi ya wanadamu yaliyobadilishwa baada ya maombi, hapo juu nimezungumzia tu mifano ya maombi yaliyobadilisha maamuzi ya Mungu. Maombi yanaweza kugeuza maamuzi ya yule bosi wako pale kazini, maombi yanaweza yakabadili maamuzi ya watawala. Maombi yanaweza kubadili matamko na laana za ukoo, inawezekana familia inapitia kwenye vifungo vya umaskini mkubwa pamoja na kufanya kazi kwa juhudi, roho za magonjwa, vifungo vya kutokuoa au kutokuolewa, kwa njia ya maombi mwamini anaweza kubadili laana zote na kuwa Baraka.

TATU: Maombi yanatupa nguvu ya kutoingia majaribuni ; Yesu aliwawaambia wanafunzi wake maneno haya kwa uzito sana baada ya kuona wanafunzi hawana maisha ya maombi! Walikuwa wanafikiri jukumu la kuomba ni la Yesu tu! Kama sisi tunavyofikiri sasa, kwamba jukumu la kuomba ni la watu fulani tu, na si la kwetu.
Kila mahali ambapo Yesu alikuwa anaomba wanafunzi wake ambao leo tunawatambua kama mitume! Walikuwa hawana maisha ya maombi. Angalia hapa Luka 9:28-32, “Baada ya maneno hayo yapata saa nane, akawatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba (Hilo ndio lilikuwa lengo lakini angalia matokeo yake).Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka…” (Hapa Yesu anaomba peke yake wale aliopanda nao walishamwacha walikuwa na usingizi). Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi: lakini walipokwisha amka…”
Inaonyesha wazi walikuwa wamelala wakati Yesu anaomba! Walikuwa wanaona shida kuomba kama sisi tunavyoona shida! Lakini tatizo lilikuwa linajirudia tena na tena kwa wanafunzi mpaka ikabidi Yesu awaambie madhara ya kutokuwa na maisha ya maombi! Hapa lilikuwa tukio jingine sio lile la mlimani! Mathayo 26:40-41, “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, je! Hamkuweza kukesha nami hata saa moja? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni.

NNE; Maombi yanaondoa vikwazo au vipingamizi vyote: “Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” (Marko 11:23-24).

TANO; Maombi hugeuza mioyo na tabia ya watu wengine; “Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka kuniomba? Basi nikamwomba Mungu wa mbinguni. Nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na ikiwa mimi, mtumishi wako, nimepata kibali machoni pako, tafadhali unipeleke mpaka Yuda, niuendee mji wa makaburi ya baba zangu, nipate kuujenga. Mfalme akaniuliza, (malkia naye ameketi karibu naye), Safari yako itakuwa ya siku ngapi? Nawe utarudi lini? Hivyo mfalme akaona vema kunipeleka; nami nikampa muda. Tena nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na nipewe nyaraka kwa maliwali walio ng'ambo ya Mto, ili waniache kupita mpaka nifike Yuda; nipewe na waraka kwa Asafu, mwenye kuutunza mwitu wa mfalme, ili anipe miti ya kufanyizia boriti kwa malango ya ngome ya nyumba, na kwa ukuta wa mji; na kwa nyumba ile nitakayoingia mimi. Naye mfalme akanipa, kama mkono mwema wa Mungu wangu ulivyokuwa juu yangu.” (Nehemia 2:4-8).

SITA; Maombi ni njia ya uponyaji wa kimwili na kiroho; “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.” (Yakobo 5:14-15).

SABA; Maombi huleta msukumo wa kiroho na kumtia mtu nguvu wakati mtu fulani anapokabiliwa na hali ya kushindwa: “Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni; mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu; mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha; (Wakolosai 1:9-11).

NANE; Maombi hufungua milango ya nguvu za Mungu zisizo za kawaida katika maisha yetu: Maombi yanaachilia mwaliko kwa Mungu wetu kutenda kazi katika ulimwengu wetu. Kwa ujumla, maombi ni njia ya kuita nguvu ya Kimungu ili ikatende kazi katika eneo kusudiwa. “Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.”(MDO 16:25-26)

TISA; Maombi ni njia Mungu aliyoichagua kuzuia nguvu na utendaji kazi wa shetani duniani; “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho… kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote (EFES. 6:12, 18)

KUMI; Kwa njia ya maombi unaweza kuwa mahali kiroho ambapo huwezi kuwa kimwili: Kwa njia ya Maombi unaweza ukasafiri mapaka mkoa mwingine na ukaenda kufanya shughuli za kihuduma huko.

KUMI NA MOJA; Maombi yanakuwezesha kushiriki maamuzi mbali mbali pamoja na Mungu kwenye ulimwengu wa roho: Lakini ndugu yangu nikuambie ukweli maombi ni njia nzuri sana ambayo unashiriki moja kwa moja maamuzi ya mambo mengi katika jamii unayoishi. Inawezekana ni katika familia, au kanisani, au kama ni mtaani kwako, kama ni katika nchi yako na kadhalika. Mungu ametuweka kama mawakili katika maeneo yetu tulipo. Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya; wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.”(ISA. 62:6-7)
WARUMI 8:28, " Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. "

KUMI NA MBILI; Kwa maombi yako ingia katika ulimwengu wa roho ili ubadili hali ya ulimwengu wa kimwili: Ulimwengu wa roho ndio mkuu zaidi kuliko ulimwengu wa mwili. Ulimwengu wa roho ndio unautawala ulimwengu wa mwili. Dunia na vyote vyenye kuonekana vimetokea kutokana na ulimwengu ule usioonekana. kila jambo linalotekea katika ulimwengu wa mwili limeanzia katika ulimwengu wa roho. Kufaulu na kushindwa kwetu kote, kabla ya kudhihirika katika ulimwengu wa mwili, kuna kuwa kumepangwa na kutekelezwa katika ulimwengu wa roho. Biblia inasema; “mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo” (3 YOH. 1:2). Hii inamaanisha kwamba mafanikio yetu ya kweli kimwili yanategemea mafanikio yetu ya kiroho. Ni katika ulimwengu wa roho ndiko tunakosimama au kuanguka, tunakoshinda au kushindwa. Adui akitaka kukudhibiti, anamdhibiti roho yako, ukishindwa kufanikiwa rohoni, huwezi kufanikiwa mwilini.

MKESHA MKESHA MKUUUBWA WA KUSIFU KUABUDU NA KUOMBA

kanisa LA FPCT SEGEREA  linawakaribisha katika mkesha mkuuubwa wa kuomba, kusifu na kuabudu
Utakao fanyika kanisani hapo ni ijumaa ya TAREHE 26 OCTOBER 2018
kuanzia saa 3:00 Usiku hadi saa10:00 Alfajiri 
Wagonjwa na wenye shida mbalimbali wataombewa kwa jina la Yesu
Usipange kukosa hii maana haijawai tokea kuna waimbaji wengi sana na kwaya na praise Team yakutosha
na ukija uje na mwenzio 
Kwa maelezo zaidi mawasiliano yapo hapo chini 



Alhamisi, 13 Septemba 2018

💐🌺🏒🌾🌴🌴KESHA LA ASUBUHI LEO SEPTEMBER 14/2018🌻🌻🌷⛅🌴ISAYA🌾🌾

💐🌺🏒🌾🌴🌴KESHA LA ASUBUHI LEO SEPTEMBER 14/2018🌻🌻🌷⛅🌴ISAYA🌾🌾


Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione. Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa. Isaya 6:9, 10.


K
azi ya Nabii huyu ilikuwa dhahiri; alipaswa kuinua sauti yake dhidi ya maovu yaliyoenea. Lakini aliogopa kutekeleza kazi hii pasipo kupewa uhakikisho wa tumaini. “Ee Bwana, hata lini?” (Isaya 6:11) aliuliza. Je asiwepo ye yote miongoni mwa wateule wako atakayeelewa, na kutubu, apate kuponywa?

Mzigo wa roho yake kwa niaba ya Yuda wanaopotoka haukubebwa bure. Utume wake usingelikosa kabisa matunda. Lakini bado maovu ambayo yalikuwa yakiongezeka kwa vizazi vingi yasingeondolewa katika siku zake. Katika maisha yake yote anapaswa kuwa mwalimu jasiri, mwenye uvumilivu-nabii wa matumaini pia wa hukumu. Kusudi la Mungu litakapotimilizwa hatimaye, matunda kamili ya juhudi zake, na ya kazi za wajumbe waaminifu wote wa Mungu, yataonekana. Masalia yataokolewa. Ili kwamba hili lipate kutokea, ujumbe wa onyo na kusihi ulipaswa kutolewa kwa waasi, Bwana alitamka, “Hata miji itakapokuwa ukiwa, haina wenyeji, na nyumba zitakapokuwa hazina watu, na nchi hii itakapokuwa ganjo kabisa; hata Bwana atakapowahamisha watu waende mbali sana, na mahame yatakapokuwa mengi ndani ya nchi” (aya 11, 12).

Hukumu nzito zilikuwa ziwaangukie wasiotubu hawa-vita, uhamisho, ukandamizaji, kupoteza mamlaka na heshima miongoni mwa mataifa-haya yote yalikuwa yaje ili kwamba wale ambao wangetambua ndani yake mkono wa Mungu waliyemkosea wapate kuongozwa kutubu. Makabila kumi ya kaskazini yalikaribia kutawanywa miongoni mwa mataifa, na miji yao kuachwa ukiwa; hata Yerusalemu hatimaye ilikuwa ianguke, na Yuda ilikuwa ichukuliwe mateka kwenda nje; hata hivyo bado Nchi ya Ahadi haikupaswa kubaki ikiwa imetupwa milele. -Review and Herald, March 11, 1915. 🌿🌿🍀BARIKIWENI

Jumanne, 4 Septemba 2018

TEMBEA KATIKA IMANI ILI USHINDE YOTE

Biblia katika kitabu cha Mathayo 17:18 inasema‘ ..Ni kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana amini nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. Hii ni habari ya yule kijana aliyekuwa na pepo bubu na kiziwi, mzazi wake akamleta kwa wanafunzi wa Yesu wamwombee. Biblia inatueleza kwamba wanafunzi walijaribu kumtoa yule pepo wasiweze, wakati huo Yesu alikuwa amepanda Mlimani kwenda kuomba. Yesu aliporudi alielezwa kilichotokea, akawakemea wanafunzi wake na kisha akamuombea yule kijana akapona. Baadaye wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo. Ndipo Yesu akawajibu akasema ‘Ni kwa sababu ya upungufu wa imani yenu… Neno upungufu lina ya isiyo – tosheleza, yaani imani yao ilikuwa ina upungufu na kwa hiyo wasingeweza kumtoa yule pepo. Jambo ninalotaka tuliangalie ni kwamba kwa kuwa tatizo lilikuwa ni upungufu wa imani yao, ina maana walitakiwa kuongeza imani yao wakati wanaendelea kukemea. Sasa swali muhimu ni je wangeongezaje imani yao wakati wako kwenye jaribu/vitani?. Naam licha ya swali hili kuna maswali mengine ambayo ni muhimu kuyatafakari ili tuweze kuwa na ufahamu mzuri wa imani. Je upungufu huu wa imani kwa wanafunzi walikuwa nao kabla hawajaanza kukemea yule pepo au ulikuja wakati wanaendelea kuomba. Naam Yesu anatuonyesha kwamba kosa la hawa wandugu wenzetu lilikuwa upungufu wa imani yao? Ni kwa namna gani walikuwa na upungufu wa imani? Biblia katika Waebrania 11:1 inaeleza kwamba ‘imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana’ . Kwa hiyo endapo Yesu alisema ni kwa sababu ya upungufu wa imani yao ina maana ndani yao walipungukiwa uhakika wa kile walichokitarajia, ambacho ni kufunguliwa/kuponywa kwa kijana mwenye pepo. Naam upungufu wao wa imani ulitokana na mashaka juu ya uhakika wa yule kijana kufunguliwa. Nini kilipelekea wao kuingiza hofu/mashaka? Kukosekana kwa dalili za kijana kufunguliwa – Ni imani yangu kwamba wanafunzi walipoanza kukemea walikuwa na uhakika kwamba Yule kijana atafunguliwa. Naam kadri walivyoendelea kuomba na kuona kwamba hakuna mabadiliko ya aina yoyote kwa mgonjwa yule ndipo hofu/mashaka yakawaingia mioyoni mwao. Maneno ya kusikia – Ikumbukwe kwamba chanzo cha imani yoyote ni kusikia (Warumi 10:17)? Kumbuka wakati wanendelea kuomba kulikuwa kuna kundi kubwa la watu ambao walikuwa wanamsubiri Yesu pamoja nao. Hivyo huenda wakati wanafunzi wanaaendelea kuomba walisikia watu wakisema, wanafunzi wa Yohana wenyewe walishindwa kumuombea, wao wataweza, wamejaribu watumishi wa kila aina wameshindwa, huyu hawezekani anasubiri kifo, naam haya yote yakapunguza uhakika ndani yao kwamba kwa jina la Yesu yule kijana anaweza kupona. Maneno yao wenyewe – Biblia haituelezi namna/approach waliyoitumia kuomba/kukemea. Huenda walianza kuomba mmoja mmoja/ au waliomba wachache na mwishowe ndipo wakaomba kama kundi. Kwenye kundi lolote kuna mengi, huenda walipokemea kwa muda kadhaa na bila kijana kuonyesha dalili za kupona baadhi ya wanafunzi wakaingiwa na hofu na wakawaambukiza na wengine na hivyo kushindwa kumtoa pepo. Hebu jaribu kufikiri mtu kama Yuda Iskariote alikuwa anafanya nini wakati wenzake wanakemea? Nini cha kufanya? Hofu/mashaka ni silaha kubwa sana ambayo Shetani huitumia kuwafanya watu washindwe kupata majibu ya maombi/miujiza yao kutoka kwa Mungu. Shetani anafahamu kwamba imeandikwa ‘Mwenye haki wangu ataishi kwa imani, naye akisstasita roho yangu haina furaha naye’ (Wabrania 10:38). Hivyo ili kuharibu/kuondoa imani ya mtu kwa Mungu, silaha anayotumia ni kuingiza mashaka moyoni mwake dhidi ya ahadi za Mungu/neno la Mungu kwenye maisha yake. Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake ‘… amini nawaambia yeyote atakayeuambia mlima huu ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake’ (Marko 11:22). Mpenzi msomaji kamwe usimruhusu Shetani kwa kutumia silaha hii ya mashaka azuie baraka zako na wale wanaokuhusu maishani mwako. Haijalishi jaribu limesimama mbele yako kwa kiwango gani usiondoe imani yako juu ya kile ambacho Yesu amekisema kwenye neno lake juu yako. Naam Mungu wetu si mtu hata aseme uongo, ahadi zake ni amina na kweli. Naam katikati ya jaribu/changamoto wewe ongeza imani yako kwa kupambana na roho ya mashaka/hofu, naam tumia Biblia ili ikuongoze kukupa mistari ambayo itakuongezea uhakika wa kufanikiwa katika lile ulifanyalo. Zaidi kuwa makini na maneno ya kusikia kwa habari ya imani yako. Wanafunzi wa Yesu walipaswa kutokujali maneno ya kusikia kutoka kwa watu, au kwa wenzao walioingia mashaka, naam walipswa kudumu kuamini kwamba kijana atapona naam ingekuwa hivyo. Je si unakumbuka habari za Petro alivyoambiwa na Yesu atembee juu ya maji. Awali alianza vema na akatembea hatua kadhaa juu ya maji. Biblia inasema dhoruba ilipompiga akaona shaka na kuanza kuzama. Kwa nini alizama? si kwa sababu Yesu hakuwepo, bali ni kwa sababu aliona shaka. Naam kitu kilichopungua kwenye imani ya wanafunzi, ni uhakika kwamba yule kijana atapona. Na kilichopelekea upungufu wao wa imani, si kutokumwamini/kumjua Yesu, bali ni kuruhusu hofu ichukue nafasi ya imani/uhakika waliokuwa nao kwamba yule mgonjwa atapona. Naam kwa mara nyingine tena ‘usirihusu hofu iharibu muujiza/future yako’ . Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nawe daima.

JIFUNZE KUENENDA KWA ROHO ILI USIMUHUZUNISHE ROHO MTAKATIFU

Shalom, hakuna namna mwamini anaweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu hapa duniani bila kuenenda au kuongozwa na Roho Mtakatifu kwani yeye ndiye aliyepewa jukumu la kutufundisha na kutuonyesha njia itupasayo kuiendea. Hivyo basi suala la kujifunza kuenenda kwa Roho ni la LAZIMA kwa kila mwamini ili aishi maisha aliyokusudiwa awapo duaniani na kuepuka matokeo ya kumhuzunisha Roho Mtakatifu maana gharama yake ni kubwa sana.
Biblia kwenye Waefeso 4:30 inasema ‘Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi’ na tena imeandikwa ‘Msimzimishe Roho’
(1Wathesalonike 5:19). Roho Mtakatifu ni Mungu, anayo nafsi ambapo ndani yake kuna hisia na kwa jinsi hiyo anaweza kufurahi au kuhuzunishwa pia (1Wathesalonike 5:6). Matokeo ya kumhuzunisha Roho Mtakatifu ni mabaya sana kwa mwanadamu na Mungu pia, ingawa mwenye kuathirika zaidi ni mwanadamu na ndio maana tunaonywa tusimuhuzunishe.
Kumhuzunisha Roho Mtakatifu ni kufanya au kusema jambo lolote lile ambalo litakatisha, kusimamisha au kuzuia kabisa utendaji au uongozi wake kwenye maisha yako. Naam kwa lugha nyingine kumuhuzunisha Roho Mtakatifu ni kumuwekea mpaka katika utendaji wake kwa kukataa uongozi, maonyo au ushauri wake unaolenga kuwezesha utekelezwaji wa kusudi la Mungu kupitia mwanadamu.
Je ni kwa namna gani mtu naweza kumhuzunisha Roho Mtakatifu?
Kwenye Isaya 63:9-10 imeandikwa ‘Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, AKAWACHUKUA siku zote za kale. Lakini WAKAASI, wakamhuzunisha Roho yake Mtakatifu; kwa hiyo akawageukia, akawa adui, akapigana nao’.
Matendo ya Mitume 7:51 inasema ‘Enyi wenye shingo ngumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote MNAMPINGA Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo’. Pia Zaburi 78:40-41 inasema ‘Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani! Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; WAKAMPA MPAKA Mtakatifu wa Israeli’ .
Maandiko haya yanatufanya tujue kwamba Roho Mtakatifu anaweza kuhuzunishwa kupitia UASI wa mwanadamu. Neno
uasi lina maana ya kupinga maelekezo au kukataa kuwa chini ya mamlaka au utawala wa Mungu na kwa jinsi hiyo ni kupingana na mamlaka husika. Kadri mtu anavyomwasi Mungu kwa njia yoyote ile ndivyo anavyomhuzunisha Roho Mtakatifu, naam ndivyo anavyotengeneza mpaka na hivyo kukata mawasiliano kati yao.
Uasi wa mwanadamu ni kikwazo au kizuizi kwa Roho Mtakatifu kumsaidia na kumuongoza katika mapenzi kamili ya Mungu. Ndio ile kusema ‘ siku zote mnampinga Roho Mtakatifu’ ( Matendo ya Mitume 7:51) ina maana kuna namna alitaka kuwasiaida, wao wakakataa usaidizi wake. Uasi unaweza kuwa kwenye neno la Mungu au maelekezo mahususi ambayo Roho Mtakatifu anampa mtu katika hatua mbalimbali za utendaji au utekelezaji wa kusudi la Mungu kwenye maisha yake.
Katika Zaburi 32:8 imeandikwa ‘Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama’ . Kwenye Yohana 14: 26 imeandikwa ‘Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia’ na Yohana 16:13 imeandikwa ‘Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake’.
Hii ni kutonyesha kwamba Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu amekusudia kuyaongoza maisha ya mwanandamu katika kusudi lake na hivyo mwanadamu hanabudi kuishi kwa kufuata uongozi wake. Sasa uasi mbaya zaidi ambao mwanandamu huufanya ni ule wa kutenda au kwenda kinyume na mapenzi au maelekezo ya Mungu kwenye maisha yake na kuamua kuyafanya yale yampendezayo yeye asijue kwamba ipo tofauti kubwa ya kiathari kati ya uasi unaohusisha mfumo rasmi wa utaratibu (procedure) na ule usiohusisha mfumo rasmi utaratibu (non-procedure).
Hebu tuone mifano kadhaa ndani ya Biblia – Dhambi ya Haruni na Miriam vs dhambi ya Haruni kutengeneza sanamu ya ndama (Hesabu 12:1-14, Kutoka 32:1-35). Pia uasi wa Ibrahimu na Sara (Mwanzo 16:1-6, Wagalatia 4:22-31). Pia unaweza ukajifunza jambo hili kupitia uasi wa Musa na Haruni (Hesabu 20:12, 27:14), Uasi wa Daudi (2Samweli 11:1-27), Uasi wa Sauli (1Samweli 15:1-35) nk.
Je upi ni ufumbuzi utakaomsaidia mwanadamu asimuhuzunishe Roho Mtakatifu? Ndugu zangu, kiwa matokeo na athari za uasi ni kubwa kiasi hicho kwa mwanadamu, basi ni lazima mwanadamu ajifunze kuenenda kwa Roho ili asimhuzunishe Roho Mtakatifu. Katika Wagalatia 5:16-18 imendikwa ‘Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria’.
Kuenenda kwa Roho maana yake kuishi kwa kuongozwa na utaratibu wa Roho Mtakatifu. Biblia katika Yeremia 31:33 inasema ‘ Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu’. Warumi 8:1-2 imeandikwa ‘Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti’ .
Zipo sheria kuu mbili zinazotaka kuongoza maisha na mwelekeo wa kila mtu dunaini. Moja ni sheria ya Roho wa uzima na ya pili ni sheria ya dhambi na mauti. Hizi ni sheria ambazo daima zinapingana na haziwezi kuja kupatana na hivyo ni uamuzi wa mwanadamu kuachagua sheria anayotaka iyaongoze maisha yake kwani mtu anapoishi kwa mojawapo ya sheria hizi sheria husika inamtenga mbali na sheria nyingine.
Kabla ya kifo cha Yesu msalabani, sheria ya dhambi na mauti inayofanya kazi kupitia mwili ilikuwa na nguvu dhidi ya torati (sheria). Torati ilikuwa ni dhaifu juu ya mwili na kwa hiyo maagizo (mahitaji) ya torati yasingeweza kutimizwa ndani ya mwanadamu. Hivyo Yesu alikuja ili aihukumu dhambi katika mwili wake, naam ili kwa njia hiyo wale waendao kwa Roho waweze kutimiza mahitaji ya sheria (Warumi 8:3-4).
Roho Mtakatifu anapokuwa ndani ya mtu kuna vitu (mafuta, hekima, nguvu, neema) anaachilia ndani au juu ya mtu husika ili kumsaidia namna ya kuenenda awapo duniani. Nasikitika kusema kwamba ‘bila kujifunza na kuwa na nidhamu ya kuenenda kwa Roho, waamini wataendelea kuwa watu wenye kulalamika kila siku huku wakipoteza fursa nyingi za mafanikio sambamba na kushindwa kuishi maisha ya ushindi hapa duniani’
(Wagalatia 5:18, Luka 4:18, 1Yohana 2:27).
Kumbuka Roho Mtakatifu anao utaratibu (sheria) ambao sharti tuujue na kuufuata ndipo tutaweza kutembea naye au kueneneda kwa Roho. Mtu anapochagua kuenenda kwa Roho, Roho Mtakatifu kutokana na nafasi yake wa wajibu wake kwetu atamuongoza mtu husika katika shauri sahihi. Naam, hata hivyo ili mtu aenende kwa Roho ni lazima; kwanza atambue nafasi ya Roho Mtakatifu (Yohana 14:17) , pili ampe kibali cha kuyaongoza maisha yake ( 1Petro 1:21) na mwisho ajue namna ya kuhusiana na kuwasiliana na Roho Mtakatifu.
Naam, nidhamu ya kujifunza na kudumu kuenenda kwa Roho itakusaidia usiseme au kufanya mambo unayotaka wewe wala kuyatafuta yakupendezayo, bali uishi sawasawa na mapenzi ya Mungu. Chagua leo kuenenda kwa Roho, nawe hutajutia maamuzi yako ya kuokoka bali ndivyo utakavyojua upendo na uweza wa Mungu katika kuwaongoza watoto wake kwenye shauri lake wawapo duniani.
Utukufu na heshima vina wewe Yesu, wastahili BWANA.

Ijumaa, 24 Agosti 2018

MKESHA MKUUBWA!! WA KUOMBA, KUSIFU NA KUABUDU

kanisa LA FPCT SEGEREA  linawakaribisha katika mkesha mkuuubwa wa kuomba, kusifu na kuabudu
Utakao fanyika kanisani hapo ni ijumaa ya TAREHE 31 AUGOST 2018
kuanzia saa 3:00 Usiku hadi saa10:00 Alfajiri 
Wagonjwa na wenye shida mbalimbali wataombewa kwa jina la Yesu
Usipange kukosa hii maana haijawai tokea kuna waimbaji wengi sana na kwaya na praise Team yakutosha
na ukija uje na mwenzio na usisahau kua wamekuandalia CHAI NA VITAFUNWA BUREEE!!!! 
Kwa maelezo zaidi mawasiliano yapo hapo chini 

USIKATE TAMAA WALA USIVUNJIKE MOYO -YOUR RAINY SEASON IS COMING!

Nilipokuwa mdogo nilikuwa namuona MAMA akichambua maharage, alikuwa anaweka *maharage mazima* kwenye sufuria ya kupikia, na *maharage mabovu* alikuwa anayatoa kisha anayatupa mbali jalalani.!
Chakushangaza.. mvua ikinyesha maharage yale yale mabovu ndio yanakuwa ya kwanza kuota na kuchipua..
Yalitupwa yakiwa mabovu yasiyofaa.. lakini yanaota.. kisha yanatoa maharage mengine mazima na bora zaidi kuliko yalivyotupwa mwanzo yakiwa mabovu! “
Hii imenifanya nijifunze kuwa ni muda/wakati tu utakao amua hatma yako.. Pia jinsi Mungu anavyokuona ni tofauti kabisa na watu wanavyokuona..
Inawezekana ukaonwa/ukajiona kama maharage mabovu leo.. lakini hakika *mvua ya Mungu* ikikunyeshea UTAOTA na kuwa wa thamani na KUZAA/KUTENGENEZA WATU WENGINE BORA ZAIDI YA WEWE..
Inahitaji wakati tuu
Uvumilivu..
Na kujua kusudi la Mungu na mawazo ya Mungu ni tofauti na ya binadamu….
USIKATE TAMAA WALA USIVUNJIKE MOYO
YOUR RAINY SEASON IS COMING
Wewe ni bora na unafaa sana.!
Kila jambo chini ya jua lina wakati wake haijalishi jinsi ulivyo leo.
Mungu awabariki na nawatakia siku njema
BARIKIWA.

HIVI UNAJUA , MTU AACHI POMBE NDIO AOKOKE, BALI AOKOKE NDIPO AACHE POMBE?

HIVI UNAJUA , MTU AACHI POMBE NDIO AOKOKE, BALI AOKOKE NDIPO AACHE POMBE?

Bwana Yesu asifiwe…
Kwa ufupi sana.
Duh! Hiyo kali kwa kweli…
Je hujawahi kusikia mtumishi akikemea watu au mtu aache pombe, kisha aokoke? Au binti akiambiwa “acha uhuni, uokoke leo. ” au hujawahi kuona mtu akilazimishwa aache kitu fulani ambacho kwa kweli ni chukizo kwa Mungu, ili aokoke! Sasa hivyo ndivyo watumishi wengi husema, na Wamesahau kwamba anayemwezesha mtu fulani kuacha dhambi au uovu ni Mungu. Kama kweli anayekuwezesha kuacha dhambi ni Mungu basi ni dhahiri kabisa unamwitaji kwanza Mungu kisha Mungu akuwezeshe kuacha dhambi. Unajua ukimuhubiria mrevi aache pombe kisha ndipo aje kwa Bwana mimi nataka nikwambie hawezi kuacha pombe na hakika utamkosa huyo mtu kwa sababu si yeye awezaye, bali Roho mtakatifu ndiye awezaye kufanya kazi hiyo isipokuwa mwenye dhambi aoneshe kuhitaji msaada huo ili asaidiwe.
Hata wewe usije ukajisifia kwamba umeacha uchafu wako uliokuwa ukifanya hapo mwanzo kwa sababu ni mjanja sana. Sio kweli! Bali pale ulipoamua ukaweka nia, Mungu akakusaidia katika hilo. Lakini ujue hata kitendo cha kufanya maamuzi hayo, Mungu alihusika sana. Kumbuka tunaokoka kwa neema kwa njia ya imani katika Kristo Yesu ( Waefeso 2:8). Kanisa la leo limewakosa watu wengi walio dhambini kwa mafundisho manyonge yanayofundishwa, na matokeo yake tumejikuta tukihubiriana sisi kwa sisi na sio kwa walio nje tuwalete kanisani. Naikumbuka ile sheria ya dini yangu ya zamani kabla ya kuokoka, kasheria kalikuwa ni kuwazuilia wadada / wanawake wowote atakaye vaa nguo fupi! .
Lakini wanaume waliachwa kwa sehemu kubwa lakini ikafika wakati na wanaume wakaandikiwa kwa wale watakaovaa vikaushi kwamba makwapa yao yakionekana watolewe nje! Ni kweli mavazi yanapaswa yawe ya heshima. Lakini sheria hizi ni za wanadamu wa dini. Sasa nikuulize kama mdada wa mataifa kakimbilia kanisani kwa Yesu,kaja jinsi alivyo akiwa na nguo fupi maana ndio maisha yake yalivyo, Je wewe wa kanisani umzuie? Ebu jijibu sasa swali hilo. Vipi ukimzuia je si sawa na kumwambia rudi huko huko kwenye mataifa? Sasa Je, unategemea kwanza abadilike ndipo aingie kanisani / kwa Yssu. Sasa ni nani wa kumbadilisha huyo ikiwa ametoka duniani na wewe u mtu wa kanisani, je unafikiri ukimwambia arudi duniani awe kwanza safi ndipo aende kwa Bwana, dunia itamvadilisha? Weeeh thubutu! Nani kakwambia kwamba anaweza kubadilika akiwa huko duniani!!!!!
Kumbe kinachotakiwa ni kanisa ndilo limbadilishe baada ya kumpokea jinsi alivyo kwa maana bila shaka hata wewe ulipokelewa jinsi ulivyokuwa, sasa iweje wewe leo uweke msimamo wa kumtaka eti mtu kwanza abadilike ndipo aokoke. Ikiwa kama mpaka mtu abadilike ndipo aokoke, basi kuokoka hakuna maana, kwa maana kuokoka ni kwa mwenye dhambi jinsi alivyo, kisha Roho atambadilisha hatua hadi hatua. Ifike wakati sasa tujitambue kwa kuwakaribisha makahaba, waabuduo sanamu n. k tuwahubirie, waokoke kisha Mungu atashughulika nao kwa kuacha mambo yao. Usifikiri mchezo kuacha jambo fulani ikiwa unalipenda, bila Mungu ni ngumu na kwa kweli haiwezekani na huo ndio ukweli wenyewe.
Wainjilisti wenzangu!
Ebu ifike wakati tuone kwamba kazi ya kumfanya mtu kuacha dhambi ni ya Mungu sio ya mwenye dhambi. Tukilijua hilo tutakuwa na ujasiri mkubwa wa kuhubiri kweli, kisha tutawapata wengi na wengi watakuja kwa Kristo. Ile elementi / tabia ya kumkemea mwenye dhambi kama ya ulevi kwa kumwambia “acha pombe nakwambia, kisha uje uokoke ” tuiche, bali tuwaambie kwamba Yesu anakupenda naye atakusaidia kuacha pombe, bali wewe njoo tu kwa Yesu uokoke.
Kwa msaada zaidi pamoja na maombezi nipigie sasa kwa namba zilizopo hapo juu.

Jumatano, 22 Agosti 2018

MKESHA MKUUBWA!! WA KUOMBA, KUSIFU NA KUABUDU

kanisa LA FPCT SEGEREA  linawakaribisha katika mkesha mkuuubwa wa kuomba, kusifu na kuabudu
Utakao fanyika kanisani hapo ni ijumaa ya TAREHE 31 AUGOST 2018
kuanzia saa 3:00 Usiku hadi saa10:00 Alfajiri 
Wagonjwa na wenye shida mbalimbali wataombewa kwa jina la Yesu
Usipange kukosa hii maana haijawai tokea kuna waimbaji wengi sana na kwaya na praise Team yakutosha
na ukija uje na mwenzio na usisahau kua wamekuandalia CHAI NA VITAFUNWA BUREEE!!!! 
Kwa maelezo zaidi mawasiliano yapo hapo chini 

JE MTU AKIFA ATAKUA HAI TENA

Ayubu 14:13-14 “ Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka! Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, Hata kufunguliwa kwangu kunifikilie.”
Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele
Leo hii wakristo wote nchini wanaungana na wakristo wengine duniani kote pamoja na wayahudi kuadhimisha sikukuu ya Pasaka, kukumbuka tukio la kusulubiwa, kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo kulikotokea miaka zaidi ya 2000 iliyopita, huku Wayahudi wakiadhimisha miaka zaidi ya 3000 Tangu walipoadhimisha Pasaka ya kwanza katika siku ya 15 ya mwezi wa Nisan kwa mujibu wa Kalenda ya kiyahudi Hapo walipookolewa kutoka Misri.
Miaka mingi sana kabla ya kufufuka kwa Yesu, mtumishi wa Mungu Ayubu aliwahi kuuliza swali la msingi sana katika maisha ya mwanadamu, swali hili ni moja ya miongoni mwa maswali ya kifalsafa, swali hili liliulizwa kutokana na hoja zilizotolewa na watu wenye hekima mbali mbali waliokuja kumtia moyo ayubu na kujiuliza swali kwanini wanadamu wanateseka, swali kuhusu mateso hata leo limekuwa ni swali kubwa sana lenye mjadala mkubwa sana katika imani mbalimbali
· Wahindu wanaamini mateso yanatokana na KARMA yaani kuishi kwa kutenda Mema wanaamini kama ukiishi vibaya utazaliwa kitu kibaya na utapata shida, na hivyo katika mzunguko wa maisha Mungu atakupa mabaya na utachelewa kufika NIRVANA yaani mbinguni kukaa na Mungu
· Wabudha wanaamini kuwa mateso yanatokana na tamaa, yaani kama mwanadamu ataishi mbali na tamaa atakuwa ameingia NIRVANA hata kama bado yuko Duniani, hivyo wao hujifunza kuridhika na kujikana na kuitesa miili yao
· Waislam wanaamini kuwa mateso ni matokeo ya Kudra za mwenyezi Mungu, yaani ni mapenzi ya Mungu kwa kadiri ya majaliwa yake
· Wayahudi waliamini kuwa mtu anaweza kupata mateso kama matokeo ya dhambi zake au za wazazi wake kutokana na Mungu alivyoahidi kushuhulika na kizazi hata ta tatu na nne cha wampendao au wanaomchukiza
· Wakristo swala kuhusu Mateso ni swala pana sana na linaweza kuwa na ufafanuzi mpana sana wa kwanini wanadamu wanateseka, hata hivyo Kiongozi mkuu wa wokovu wetu yaani Yesu alikamilishwa kwa njia ya mateso
Katika kitabu cha Ayubu ni wazi kuwa Ayubu pamoja na rafiki zake walikuwa wakijadili kuhusu Mateso na sio mateso ya kawaida bali mateso ya mtu aliyeishi kwa haki, Ayubu ambaye inasemekana kuwa aliihi maisha ya hali alikuwa anateseka sana na hakuwa amepata tiba, licha ya mali yake kuwa imetekekea, licha ya kuwa amepoteza watoto wake wote, pia alikuwa na majipu mabaya yaliyokuwa yakifumba na kufumbuka mwili mzima kutoka kichwani hata unyayoni, Ayubu na wenzake walikuwa wamejadili na kutafuta suluhu bila kupata ufumbuzi na hivyo Aybu alikuwa anatazamia kufa aliamini kuwa sasa hakuna tumaini lingine lililosalia zaidi ya kifo tu, ndipo Ayubu akauliza katika hali yakukata tamaa
Kwamba mbona miti ikikatwa shina lake huchipuka? Na maji ya bahari hupwa na kujaa ni kama inaonekana kuwa viumbe hivyo vina matumaini lakini sivyo ilivyo kwa mwanadamu, inaonekama kama mtu akifa ni mwisho wa kila kitu na hakuna matumaini ya kurejea tena, Ayubu anamwambia Mungu kwa kuwa siku za mwanadamu za kuishi ni chache na zimejaa taabu, ni afadhali angewaacha tu bila kupata mateso maana hawatakuwako tena, Hata hivyo Ayubu alikuwa na imani kuwa iko namna atamuona Mungu tu hata kama mwili wake utaharibiwa alikuwa na imani kuwa macho yake yatamuona tu
Ayubu 19: 25-27 “Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu; Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.”
Swali lililoulizwa na Ayubu Mungu aliwahi kumuuliza mtumishi wake Ezekiel katika namna nyingine,
Ezekiel 37:1-3 “. Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa; akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana. Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe ”.
Wakati huu taifa la Yuda lilikuwa limechukuliwa utumwani Babel na kila kitu iimeaharibiwa na kufa hakukuwa na matumaini ya uhai tena ndio maana swali hili lilikuwa Gumu kwa Ezekiel yeye alijibu tu kuwa Bwana unajua wewe! Mtu awaye yote anapopitia katika mateso na huzuni na kukata tamaa huwa anafikiri kuhusu kurejeshwa tena katika hali aliyokuwa nayo mwanzoni your Golden Age!
Mtume Yohana ndiye mtume aliyeteseka sana kuliko mitume wote, inasemekana aliwahi kuviringishwa katika yasi na kuwashwa moto lakini alitoka akiwa safi, aliwahi kuchemshwa katika pipala mafuta ya lami lakini alitoka akiwa hai, alishuhudia wenzake na wakrito wengine wakifa na kuawa kwa kuliwa na simba kuchomwa moto na kadhalika yeye kutokana na kushindikana kufa waliamua kumpeleka katika kisiwa cha Patmo ili akateseke huko maisha yalikuwa ni yenye kuhuzunisha na kukatisha tamaa, Yesu alimuona Yohana akiwa amekata tamaa na alimpa ujumbe mkubwa wa kutia moyo
Yohana 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu .”
Swali la muhimu la kujiuliza ni kwanini Yesu alijitambulisha kuwa yu hai yaani amefufuka? Ni muhimu kufahamu kuwa ujumbe muhimu kwa mtu ANAYETESEKA, ALIYEKATA TAMAA , na ALIYE KATIKA HALI YA KUFA ni UJUMBE WA UFUFUO Yesu alifahamu kuwa huu ndio ujumbe pekee unaoweza kumpa mtu tumaini Jipya!
Habari njema kwa ndoa iliyokufa sio kuolewa tena ni kurejea tena kwa furaha iliyotoweka na upendo uliotoweka katika ndoa yake.
Tunapoisheherekea pasaka na kukumbuka kufufuka kwa Bwana wetu Yesu ni ujumbe wa matumaini
kwamba Bwana Yesu alikufa na akafufuka na kuwa mauti haimuwezi na kuwa ni yeye ndiye mwenye funguo za mauti na kuzimu, ki msingi Yesu anajibu la swali la Ayubu kuwa mtu akifa atakuwa hai tena Yesu anajibu swali hili kuwa ndio mtu akifa anaweza kuwa hai tena na anatutangazia wazi kuwa yeye anazofunguo za mauti na kuzimu na hivyo anauwezo wa kufufua matumaini yaliyotoweka kwako, anauwezo wa kufufua huduma yako, anauwezo wa kurejesha watoto wako, ana uwezo wa kurejesha kila kilicho haribiwa na kuuawa na ibilisi, ana uwezo wa kurejesha na kufufua taifa linalomtumaini yeye, Pasaka hii mimi sihitaji habari nyingine yoyote nahitaji kusikia habari za matumaini ya kuwa Yesu Kristo yuko hai na ndiye mwenye Mamlaka ya kifo na uzima na ana uwezo wa kufufua ndoto zetu, maisha yetu, matumaini yetu, uzima wetu, mimi sihitaji waraka wa maaskaofu nahitaji kumuona mteteaji wangu akisimama kiunitetea dhidi ya kila aina ya unyonge na utumwa Pasaka ina uhusiano na ukombozi nahitaji kumuoja Yesu akinikomboa mimi na familia yangu na watu wangu na taifa langu hii ndio habari njema ya ujasiri kuwa mauti haina nguvu katika maisha yetu, imepoteza mamlaka ni yesu pekee mwenye mamlaka hiyo yeye atafufuka pamoja na mashaka yangu yeye atahuisha nafsi yangu!

PEMBE YA WOKOVU NI NINI

Mstari wa Msingi: Zaburi 18:2-8 “Bwana ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na PEMBE YA WOKOVU wangu, na ngome yangu.
YQNitamwita Bwana astahiliye kusifiwa, Hivyo nitaokoka na adui zangu. Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu. Kamba za kuzimu zilinizunguka, Mitego ya mauti ikanikabili. Katika shida yangu nalimwita Bwana, Na kumlalamikia Mungu wangu. Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake, Kilio changu kikaingia masikioni mwake. Ndipo nchi iliyotikisika na kutetemeka, Misingi ya milima ikasuka-suka; Ikatikisika kwa sababu alikuwa na ghadhabu. Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto ukatoka kinywani mwake ukala, Makaa yakawashwa nao.”
Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-
1. Maana ya neno Pembe
2. Maana ya pembe ya wokovu
Maana ya neno Pembe.
Neno Pembe ya wokovu limetajwa mara nytingi sana katika sehemu mbalimbali za Maandiko Matakatifu yaani Biblia, Lakini itakuwa muhimu zaidi kama tutafahamu kwa pamoja kwa kina na mapana na marefu maana ya Pembe ya wokovu, neno Pembe na uhusiano wake katika wokovu.
Neno Pembe katika Biblia waebrania wanaiita “ SHOFAR” imetumika katika maandiko kuelezea mambo mengi sana, katika namna nyepesi wote tunafahamu kuwa Pepmbe ni aina mfupa mgumu unaojitokeza na kukua katika kichwa cha mnyama, Mwanzo 22:13 , Pembe ya mnyama hususani kondoo mume inatumika kama silaha ya Kushambulia, Kulinda, kuonyesha mamlaka na utawala na kuleta Hofu, ni ishara ya nguvu, uweza na ushindi, kwa Msingi huo maandiko yanapotaja Pembe mara nyingi hutumika kuelezea uweza na nguvu.
Kwa lugha nyingine ya kinabii neno Pembe pia linatumika kuelezea kuhusu Serikali, au ufalme au nguvu ya dola yaani nguvu za ufalme huo unaweza kuona katika Daniel 7:7, 24 “ Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.; 24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Unaweza kuona hivyo Pembe huzungumzia NGUVU au uweza wa KIJESHI Dolla, kwa msingi huo taifa au kabila fulani linapoondolewa ngvu zake lugha ya kibiblia maana yake pembe zake zimekatiliwa mbali Yeremia 48:25 “Pembe ya Moabu imekatika, na mkono wake umevunjika, asema Bwana. Mlevyeni; kwa maana alijitukuza juu ya Bwana ”
Pembe pia hutumika kuelegea nguvu ya Upako yaani uwezo wa Roho Mtakatifu,Pembe katika agano la kale zilitumika pia kuweka mafuta maalumu ya upako ambao wangepakwa watu kama makuhani, manabii na wafalme kwa kusudi la kutimiza mapenzi ya Mungu mfano 1. Samuel 16:1-3 “ Bwana akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe. Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi Bwana akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea Bwana dhabihu. Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako, 13 Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama .” Aidha Pembe zilitumika kama tarumbeta za kumsifu Mungu na zilipopulizwa pembe kwaajili ya utukufu wa Mungu ngome za adui zilianguka na kusambatratika kabisa Yoshua 6:1-5 “ Basi Yeriko ulikuwa umefungwa kabisa kwa sababu ya wana wa Israeli; hapana mtu aliyetoka wala hapana mtu aliyeingia. Bwana akamwambia Yoshua, Tazama, nimeutia Yeriko katika mkono wako, na mfalme wake, na mashujaa wake. Nanyi mtauzunguka mji huu, watu wote wa vita, mkiuzunguka mji mara moja. Fanya hivi siku sita. Na makuhani saba watachukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume, mbele ya hilo sanduku; na siku ya saba mtauzunguka mji mara saba, nao makuhani watapiga tarumbeta zao. Kisha itakuwa watakapopiga hizo pembe za kondoo waume kwa nguvu, nanyi mtakaposikia sauti ya tarumbeta, watu wote watapiga kelele kwa sauti kuu; na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale, na hao watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele kukabili. ”
Tafasiri nyingine ya kibiblia ilihusu pembe za madhabau kwa maana ya kuwa kila kona ya madhabau kulikuwa na pembe nne, pembe hizi zilivyunyiziwa damu wakati wa kutoa dhabihu ili kwamba watu waweze kufanyiwa upatanisho kwa mungu na kupata rehema, sehemu hii ya pembe pia ilitumika kwa ibada ya upatanisho kati ya Mungu na wanadamu Walawi 8:15 “ Kisha akamchinja; na Musa akaitwaa damu yake, akaitia katika pembe za madhabahu pande zote kwa kidole chake, akaitakasa madhabahu, kisha akaimwaga hiyo damu hapo chini ya madhabahu, na kuitakasa, ili afanye upatanisho kwa ajili yake.” Eneo hili la pembe za madhabahu lilitumika pia kumaanisha MAKIMBILIO au kujisalimisha endapo mtu angekuwa na tatizo linalohitaji kujihami, au kujitakia rehema hususani alipataka kuuawa 1Wafalme 1:50 “Adonia naye akaogopa mbele ya Sulemani; akaondoka, akaenda, akazishika pembe za madhabahu .” Kwa hivyo kimsingi hizo ndizo maana ya Pembe kibiblia.
Maana ya Pembe ya wokovu!
Kama tulivyoweza kuona kwa uapana na kina na urefu kuhusu maana ya neno Pembe sasa ni muhimu kwetu tukarejea katika andiko letu la Msingi Zaburi 18: 2 “ Bwana ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na PEMBE YA WOKOVU WANGU, na ngome yangu.” Hapo sasa utaweza kumuelewa vema mwandishi wa zaburi anapozungumzia kuhusu Pembe ya wokovu wake, kwamba ana maanisha nini, Pembe kwa msingi huo ilitumika kuelezea WOKOVU neno wokovu katika kiyunani ni SOTERIA ambalo maana yake ni Nguvu ya kuweka Huru, Nguvu ya kukuondoa Hatarini, Nguvu ya kukulinda na Hatari, Nguvu ya ukombozi, Nguvu ya kuharibu mipango ya adui, Nguvu ya kusambaratisha nguvu za adui yako Zaburi 75:10 “ Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka” Kazi hii ya ukombozi Israel walikuwa na ufahamu na Roho Mtakatifu aliwafunulia wazi kuwa Dola hii au nguvu au serikali hii inayoweza kuleta ukombozi, inayoweza kuvunja vunja nguvu za adui zako, inayoweza kuharibu kila aina ya nguvu za upinzani, inayoweza kukulinda, inayoweza kukuokoa, inayoweza kukupa rehema na neema, inayoweza kukutetea dhidi ya adui zako dhidi ya waliokudhulumu, dhidi ya waonevu, dhidi ya magonjwa, dhidi ya masononeko, dhidi ya ufisadi, dhidi ya fitina, faraka , masengenyo mateto kunenwa vibaya, kusingiziwa, kuvunja nuksi mikosi na balaa, kukuweka huru nguvu hii inaitwa PEMBE YA WOKOVU
LUKA 1:67-75 “. Na Zakaria, baba yake, akajazwa Roho Mtakatifu, akatabiri, akisema, Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa. Ametusimamishia pembe ya wokovu Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake. Kama alivyosema tangu mwanzo Kwa kinywa cha manabii wake watakatifu; Tuokolewe na adui zetu Na mikononi mwao wote wanaotuchukia; Ili kuwatendea rehema baba zetu, Na kulikumbuka agano lake takatifu; Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu, Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu, Kwa utakatifu na kwa haki Mbele zake siku zetu zote .”(my god mya god ribasakarabashanda! Rebosokoroboshi ribabababaskataritoli yenderebekisha sanda) Zekaria akajazwa Roho Mtakatifu kwa msingi huo maneno hayo ni ya Roho Mtakatifu, Na hapo yanamtaja “ YESU KRISTO” ndni yake kuna ukombozi, ndani yake kuna kuokolewa na adui zetu ndani yake kuna kutolewa mikononi mwa wanaotuchukia Mungu wangu, kumbe kwaajili ya amani yetu na ulinzi wetu hatuhitaji pembe za waganga wa kienyeji, kwa sababu tunayo pembe tumesimamishiwa Pembe ya wokovu, Jina Yesu maana yake ni wokovu, Yesu ni mwenye nguvum kama zilivyo nguvu za Pembe za wanyama wakali, wenye nguvu Yuko mwenye nguvu kuliko vyote yeye ni pembe ya wokovu wangu, yeye ndio kimbilio letu yeye ndio mahali sahihi pa kujisalimisha mmmmmhmmmm my God najisikia kuhubiri hapa kuna mtu nasema naye hapa viti haviwezi kukalila maana nimempata Yesu, nimepata nguvu nina upako nina ulinzi wa ajabu sio kitu kingine ni Yesu mwana wa Mungu aliye hai pambe ya wokovu wangu!
Mungu akubariki tafadhali si mbaya ukinijuza jinsi ulivyobarikiwa na somo hili sms or whatsapp 0628080839