KAZI YA YESU YA WOKOVU.


=Mungu wangu aendelee kukubariki sana kwa kuendelea kuwa mfuatiliaji mzuri wa masomo haya ambayo bado tunayo safari nzuri tu ya kuendelea kujifunza siri hizi za ufalme wa Mungu.

=Bado tupo kwenye eneo hili la kazi ya Yesu ya wokovu, tukiwa mwishoni mwishoni kabisa ninaamini Bwana ni mwema kwa ajili yetu anachotaka tukijue safari hii lazima tukipate hakika.

=Kipindi kilichopita tulipata nafasi ya kuangalia eneo kidogo tu kuhusu kifo cha Yesu, kwamba kwanini ilibidi kiwe cha msalaba na sii vinginevyo.

=Leo nataka tuangalie kuzikwa kwake na kukaa kaburini siku tatu na mwishowe kufufuka, kuna siri kubwa hapo.
 *KUZIKWA KWAKE.*
=Kimsingi siongelei kile kitendo cha kuzikwa bali ninaongelea ule muda tangu aisalimu roho yake hadi alipofufuka siku ya tatu kama alivyosema.

=Kwanza kabisa niweke sawa hapa, Yesu hakukata roho bali aliitoa/aliisalimu roho yake, kwa maana kwamba Yesu kwa sababu ni Mungu hakuna mwanadamu ambaye angeweza kumwondoa uhai wake lakini alikubali mwenyewe kuutoa kisha akaja kuurudisha tena.

=Japo ukisoma kwenye tafsiri yetu ya Kiswahili injili ya Marko na Luka waliandika kwamba alikata Roho, lakini ukienda kwenye tafsiri za awali za biblia ya King James old version inasema wazi kwamba aliitoa roho yake na siyo kukata Roho.

=Injili ya mathayo na Yohana yenyewe ilitafisiriwa vizuri hilo neno; Mathayo alitimia neno kutoa uhai, la Yohana ametumia neno kuisalimu Roho, ambazo zote hizo zimekaa vizuri kama tafsiri za awali zilivyo.

=Hebu angalia hapa;
Yoh 10:17-18 *“Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu”*

=Ninaamini tuko sawa mpaka hapo.

=Sasa kilitokea nini katika ulimwengu wa roho wakati Yesu akiwa amekufa?

#Kwanza kabisa, kuanzia saa sita hadi saa tisa kabla Yesu hajaitoa roho yake kulikuwa na giza nchi yote maandiko yanasema hivyo; hiyo ilikuwa ni ishara kama ulimwengu wa giza umeshinda lakini dakika chache baadaye baada ya Yesu kuitoa Roho yake wakatu huo huo;

@tetemeko kubwa likatokea juu ya nchi,
@miamba ikapasuka,
@pazia la hekelu likapasuka kuoka juu hadi chini
@na cha kushangaza zaidi miili ya watakatifu wa kale waliyokuwa wamekufa wakafufuka tena wakawatokea wengi huko Yerusalemu.

=Hebu angalia maandiko;
Mathayo 27:50-53 *“Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”*

=Siwezi nikaelezea kila kitu lakini nimelenga zaidi kwenye pazia kupasuka la kupaingia patakatifu hadi patakatifu pa patatakatifu, hapa ilikuwa inaonyesha sasa kwamba njia iko wazi kwa kila mmoja atakayeoshwa nah ii damu ya Yesu kuingia patakatifu kwa sababu naye ni kuhani.

=Lakini pia ilionesha kwamba Yesu aliye kuhani mkuu aliingia na damu yake mwenyewe hadi patakatifu pa patakatifu na kuinyunyizia kwenye kiti cha rehema ili kufanya upatanisho wa Mungu na manadamu wote watakao mpokea.
 Haya yalifanyika ndani ya hizi siku tatu Yesu akiwa kwenye uso wa nchi kama maandiko yasemavyo;

2Wakor 5:19 *yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.*

=Kuna kitu kingine cha ajabu hapa; mwanzoni kabla Yesu hajafa watu wote waliyokuwa wanakufa walikuwa wanaenda sehemu moja iliyokuwa imetenganishwa iliyoitwa kuzimu ambayo hadi sasa kuzimu ipo na ndiyo makao ya shetani na roho zote ovu pamoja na roho za wanadamu waliyokufa katika dhambi.

=Kabla ya Yesu ilikuwa kwamba ukifa mcha Mungu unaenda mahali palipoitwa kifuani mwa Ibrahimu ambako hakuna mateso badala yake ni raha tu, kulikuwa na shimo kubwa lililowatenga ambapo upande wa pili ndipo kuzimu kwenyewe ambako roho za wenye dhambi huenda kuteseka wakisubiri hukumu ya mwisho.

=Ndiyo maana kama unakumbuka Yesu alitoa mfano wa Tajiri na Lazaro namna walivyoishi duniani na maisha yao baada ya haya ya duniani.

=Sina muda lakini naomba usome kwa utulivu LUKA 16:19-31, *utakutana na kisa hiki. Ndiyo hali halisi ilivyokuwa kabla ya Yesu hajafa.*

=Ni nini kilitokea Yesu alipokufa?

=Tumesoma hapo kwamba miili ya watakatifu iliinuka kutoka makaburini tena hata hao waliyofufuka wakawatokea watu na kuuingia mji mtakatifu yaani Yerusalemu.

=Yesu naye alipokufa kama mwanadamu wa kawaida roho yake ilishuka kuzimu, na alipofika kuzimu kwenye eneo la wenye haki au watakatifu kama naye alivyokuwa mtakatifu akawatoa wote kuzimu ili awahamishie makao yao, ndiyo maana biblia inasema ilifufuka miili ya watakatifu peke yao.

=Ndiyo akaihamishia mahali pengine paitwapo paradiso ambapo ni juu wala siyo mbinguni lakini ni mahali pa raha ambapo watakatifu wanapokufa wanaishi hapo wakisubiria kufunuliwa kwa Yesu mara ya pili.

=Ndipo akaenda upande wa pili wa kuzimu ambapo ndipo makao ya shatani na roho za wanadamu waatenda dhambi waliyokufa ambako pia kuzimu maana yake ni kifungoni, na Yesu akaenda kuwahubiria huko siyo ili waokoke bali akawaeleza kwamba yeye ndiye aliyekuwa anahubiriwa na manabii na torati.

=Najua unashangaa hii hujawahi kuishikia lakini nakufundisha biblia, hebu angalia hii;

1Petro 3:18-20 *“Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni (kuzimu), akawahubiri; watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”*

=Lakini baada ya hapo akamfuata Shetani ndipo akamnyang’anya ufunguo wa mauti na kuzimu, ikimaanisha sasa mauti haina nguvu wala kuzimu kwa wale wote wanaomwamini Yesu.

=Hizi ni siri za ndani kabisa ningeweza kukueleza mengi zaidi lakini Bwana atatupa wakati mwingine kuyachambua haya, hii nimekupa ili ikupe ujasiri na kujijua nafasi yako ilivyo ya thamani katika Kristo Yesu wewe uliyeokoka na kama bado nakupa nafasi kabisa unifuate inbox nitakuongoza vyema tena nitakuwa tayari kukusimamie hadi ukuo kiroho.

Maoni