KUFUFUKA KWA YESU.
=Yesu baada ya kukaa kwenye uso wa nchi huku akishughulika kuhakikisha wokovu unapatikana kwa watu wote watakao mwamini kama tulivyoona baadhi ya mambo muhimu Yesu aliyoyafanya kwenye ulimwengu wa roho, hatimaye siku ya tatu alifufuka.
=iyo tu kwamba alifufuka lakini yuko hai milele na milele na mauti haina nguvu juu yake tena,
=Yesu ni mwanadamu pekee hadi leo ambaye kaburi lake liko wazi, kwa sababu kama ni kufufuka tu siyo hoja, kuna watu wengi katika historia walifufuka lakini baada ya muda walikufa tena.
=Kufufuka kwa Yesu kuna umuhimu gani kwetu?
=Siwezi kwa leo nikaelezea mambo yote yaliyotokea ya ajabu kwa sababu ya Yesu kufufuka, lakini labda nikuoneshe kitu hapa;
=Kwanza kabisa imani yetu ina nguvu sana kwa sababu Yesu japo alikufa lakini alifufuka na akawa hai milele na milele.
=Yaani kama Yesu asingalifufuka imani yetu ingekuwa bure na asingekuwa na utofauti na waanzilishi wa dini zilizopo hapa duniani tunazozifahamu kama Muhamedi wa dini ya kiislamu na wengineo ambao hata sasa bado wamelala makaburini.
=Hebu angalia hii:
1Wakor 15;14 *“tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure”
Isitoshe hapo chini kwa msisitizo ikarudiwa;*
1Wakor 15;14 *“tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure”
Isitoshe hapo chini kwa msisitizo ikarudiwa;*
1Wakor 15;17 ” Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu”
=Yesu alipofufuka ni nini kilitokea?
=Jambo kubwa sana lilitokea kiroho kwa sababu kwa kufufuka kwake aliishinda mauti ambayo ndiyo ilikuwa inafanya kazi kwenye maisha ya mwanadamu kwa sababu ya dhambi.
=Tena mauti ninayoiongelea hapa ni mauti ya kiroho ambayo ni kutengwa na Mungu milele.
=Kwa hiyo mwili wake ulifanyika limbuko (mzaliwa wa kwanza) kwa ajili ya wote wanaomwamini Yesu kwa hata wakipatwa na mauti ya kimwili lakini bado watafufuliwa tena na kuvikwa miili ya mbinguni na waishi milele na milele kama mwokozi wao.
1Wakor 15:20-23 “Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja”
=Kama unakumbuka tuliona kwamba Yesu pia anaitwa mzaliwa wa kwanza wa waliyokufa, ikimaanisha kwamba yeye ndiye mtangulizi kwa ajili ya wengi waliyokufa katika yeye kwamba siku moja nao watafufuka kama yeye.
=Hebu angalia tena hapa;
1Wakor 15:55-57 “Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako? Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo”
1Wakor 15:55-57 “Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako? Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo”
=Kuna mambo mengi sana hapa ya kujifunza na ninajua tutaendelea kuyaona zaidi, lakini kwa sasa angalau uwe na haya maarifa na taarifa hizi zikusaidie kujua mambo yaliyotendeka siku ulipookoka na wewe ambaye hujaokoka bado Bwana ana haja nawe tafadhali kama ukiwa tayari nione inbox au mwone mtumishi yeyote wa Mungu unayemwamini akusaidie.
Maoni
Chapisha Maoni